
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya (katikati) akikagua mfumo wa umwagiliaji bustani za mbogamboga katika maonesho yanayoendelea ya nanenane kanda ya nyanda za juu kusini jijini Mbeya.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akipokea maelezo kutoka kwa wataalam wa Chuo cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST) juu ya gari iliyotengenezewa mfumo wa nishati ya gesi katika maonesho ya nanenane kanda ya nyanda za juu kusini jijini Mbeya.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akikagua bidhaa mbalimbali kwenye banda la Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi katika maonesho ya nanenane kanda ya nyanda za juu kusini jijini Mbeya. Mkuu huyo wa Mkoa ameridhishwa na vifungashio vingi vilivyotumika katika maonesho hayo mwaka huu na wajasiriamali wa Mkoa wa Rukwa.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akiangalia "shamba jiko" ambalo staili yake ni ya kupanda mbogamboga nyumbani katika eneo dogo kwenye maonesho ya nanenane kanda ya nyanda za juu kusini jijini Mbeya.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akikagua maji aina ya Dew Drop, maji pekee yanayotengenezwa Mkoani Rukwa Mjini Sumbawanga na Mjasiriamali wa ndani, maji ambayo wananchi na wadau wengi wanasifia ubora wake kuwa ni ya kiwango cha juu. Kushoto ni Katibu Tawala Mkoa huo Alhaj Salum Mohammed Chima.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya na Katibu Tawala Mkoa huo Alhaj Salum Mohammed Chima wakikagua banda la Halmashauri ya Manispaa Sumbawanga ambalo limesifika kwa umaridadi wake.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akikagua samaki mbalimbali waliopo katika moja ya banda la Wilaya ya Nkasi katika maonesho ya nanenane kanda ya nyanda za juu kusini jijini Mbeya. Samaki hao wamekaushwa kitaalam na wana uwezo wa kukaa mda mrefu bila kuharibika.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya na Katibu Tawala Mkoa huo Alhaj Salum Mohammed Chima wakipata maelezo kwa mtaalam wa hali ya hewa walipotembelea kituo cha hali ya hewa kilichopo katika maonesho hayo. Kifaa kinachoonekana kinatumika kupima wingi wa mvua.

TanSeed wakitangaza bidhaa zao za mbegu kwa staili ya aina yake.

Ebony Fm Radio ya nyanda za juu kusini ambayo makao makuu yake ni Mjini Iringa ikifanya mahojiano ya moja kwa moja na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya mara baada ya kiongozi huyo kuzungukia mabanda kuzungumzia maonesho hayo kwa ujumla wake.

Picha ya pamoja kati ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya na baadhi wafanyakazi wa Radio ya Ebony FM ya Mjini Iringa maara baada ya Interview.