
Makamu bingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), Timu ya Azam Fc, wameanza rasmi ziara ya mechi za kirafiki nchini Afrika Kusini, ambapo leo watakuwa na kibarua kigumu cha kuumana katika mchezo wake wa kirafiki na Kaiser Chiefs ambayo inacheza Ligi Kuu ya nchi hiyo (PSL).
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Azam, Jaffer Idd, aliyefutana na timu hiyo, mechi hiyo inachezwa jijini Johannesburg, leo jioni. Kwa mawasiliano zaidi, Jaffer Idd anapatikana kwa namba +27788847399.