Quantcast
Channel: MWINYI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 3319

MSTAHIKI MEYA JERRY SILAA AKABIDHI MSAADA WA TAA ZA THEATER ZENYE THAMANI YA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI SITA HOSPITALI YA AMANA

$
0
0

Picha juu na chini Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Mh. Jerry Silaa akikabidhi rasmi msaada wa taa hizo kwa Mganga Mkuu wa Hospitali ya Amana Dk.Meshack Shimwela kwenye hafla fupi iliyofanyika hospitalini hapo.


Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Mh.Jerry Silaa akiongozana na Mganga Mkuu wa Hospitali ya Amana Dk.Meshack Shimwela (kulia) kuelekea kukagua chumba cha upasuaji katika hopspitali hiyo.


Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Mh.Jerry Silaa kupitia wadau wake ametoa msaada wa taa hizo zenye thamani ya shilingi Millioni sita laki saba na tisini elfu 6,790,000/= ambapo msaada huu wa taa umefika kwa wakati muafaka utakaowawezesha madaktari kuwahudumia wagonjwa wengi na kupunguza msongamano mkubwa wa wagonjwa wanaohitaji huduma hiyo ambao kwa hakika walilazimika kufanya pasuaji muda wa mchana peke yake hali ambayo ilisababisha msongamano wa wagonjwa hospitalini hapo.


Kwa upande wa huduma ya upasuaji hospitali ya Amana inahudumia wagonjwa kati ya 20 mpaka 30 kwa siku kwa kutumia theater mbili ambazo ni main theater na maternity theater zenye vyumba vinne vya upasuaji (theater rooms). Kwa muda mrefu Hospitali hiyo ilikuwa inakabiliwa na tatizo la kuharibika kwa taa ya upasuaji (operating lamp) ambayo imepelekea kutumia vyumba vitatu vilivyopo theater kubwa (Main theater).

Viewing all articles
Browse latest Browse all 3319

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>